Lissu amtaka Rais Magufuli ashiriki mdahalo wa televisheni
Lissu amtaka Rais Magufuli ashiriki mdahalo wa televisheni
Kiongozi wa upinzani nchini Tanzania Tundu Lissu amemtaka Rais John Magufuli ashiriki kabla ya uchaguzi mkuu wa mwezi Oktoba.
Rais Magufuli anawania muhula wa pili wa miaka mitano, huku hofu ikiendelea kuongezeka ya ukandamizaji dhidi ya vyama vya upinzani.
Bado Bwana Magufuli hajajibu kuhusu wito huo kutoka kwa Lissu.
Hii si mara ya kwanza kwa Bwana Lissu kumtaka Rais Magufuli ashiriki mdahalo wa wagombea wa urais.
Bwana Lissu, ambaye ni kiongozi wa chama cha upinzani Chadema, alisema kuwa mdahalo wa televisheni wa wagombea wa urais utakuwa ni "afya kwa demokrasia ya nchi hiyo".
Aliuambia mkutano wa kampeni kwamba rais hapaswi kuogopa kufanya mdahalo na mtu ambaye hajawahi kuwa rais kama yeye.
Alituma picha ya video hii katika mkutano wa kampeni:

Comments
Post a Comment