Mwanamume aliyekuwa amebeba cocaine kwenye makalio bandia ashikwa Ureno

Mwanamume aliyekuwa amebeba cocaine kwenye makalio bandia ashikwa Ureno


Picture shows the drug hidden in the suspect's underwearHaki miliki ya pichaPOLÍCIA JUDICIÁRIA
Image captionMwanamume aliyekuwa amebeba cocaine kwenye makalio bandia ashikwa Ureno
Polisi nchini Ureno wamemkamata mwanamume mmoja kwenye uwanja wa ndege huko Lisbon, ambaye alikuwa amebeba kilo moja ya cocaine kwenye makalio bandia.
Vyombo vya habari nchini humo vilisema kuwa raia huyo wa Brazil aliwasili kwa ndege kutoka mji wa Belém do Pará, kaskazini mwa Brazil.
Haijulikani ni vipi polisi walifanikiwa kugundia hilo.
Mwanamume mwingine ambaye anashukiwa kuwa angepokea dawa hizo alikamatwa kwenye kituo cha treni cha mji huo.
Wanaume hao watakabiliwa na kesi ya ulanguzi wa madawa ya kulevya.
Mwezi uliopita polisi nchini Ureno na Uhispania walikamata cocaine ndani ya mananasi yaliyokuwa yamessfirishwa kutoka Amerika ya Kusini.
  

Comments

Popular posts from this blog

Differences between Gymnosperms and Pteridophytes

Familia ya mwanafunzi Akwilina yataka haki itendeke