Wachezaji wa Uingereza wana tabia mbaya: Wenger




LYIMO BLOG.


Arsene Wenger alalama huu ni mchezo mchafu


Kocha wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amelalamika kwamba wachezaji wa Uingereza wamekuwa na tabia ya kujirusha na kutengeneza adhabu. Amesema mchezaji wa Tottenham Dele Alli alifanya kitendo hicho kwenye mchezo wa jumapilihuko Liverpool na kusababisha mwamuzi kutoa adhabu ya penati.
Mchezaji mwingine ambaye anatuhumiwa kufanya kitendo hicho ni Harry Kane, alifanya hivyo kwa mchezaji Virgil van Dijk wa Liverpool na kusababisha faulo pia.
Wenger amesisitiza kwamba anakumbuka kumekuwa na kesi za wachezaji kutoka nje ya Uingereza, lakini wachezaji wa uingereza sasa wameiga tabia hiyo na wamekuwa vinara wa matukio hayo kuliko wachezaji wengine.

Comments

Popular posts from this blog

Mwanamume aliyekuwa amebeba cocaine kwenye makalio bandia ashikwa Ureno

Differences between Gymnosperms and Pteridophytes

Familia ya mwanafunzi Akwilina yataka haki itendeke