HII NDIO MAANA HALISI YA WIKI KUU KWA WAKRISTO WAKATOLIKI
HII NDIO MAANA HALISI YA WIKI KUU KWA WAKRISTO WAKATOLIKI WA AMBAO HAWAJUI RATIBA YA WIKI HII KUU YA MATESO YA BWANA WETU YESU KRISTO KATIKA LITRUJIA YA KANISA, IKO KAMA IFUATAVYO:- 1. JUMATATU KUU Hii ni siku maalumu ambayo Yuda anajitoa mwenyewe kabisa katika Jumuiya ya Mitume, na kuanza mipango yake kabambe ya kumuuza Yesu. 2. JUMANNE KUU Hii ndiyo siku ambayo Yuda anatimiza mipango yake ya kumsaliti Yesu na kukabidhiwa vipande thelathini (30) vya fedha. 3. JUMATANO KUU Hii ndiyo siku ambayo Yesu anawajulisha na kuwatangazia Mitume wake juu ya mpango wa Yuda, japo kwa mafumbo na kueleza waziwazi yale yatakayompata. 4. ALHAMISI KUU Hii ndiyo siku ambayo, wakati wa jioni Yesu anaweka sakramenti kuu mbili ambazo ni: EKARISTI TAKATIFU na DARAJA TAKATIFU pamoja na AMRI KUU YA MAPENDO. 5. IJUMAA KUU Hii ndiyo siku ambayo, asubuhi na mapema (Alfajiri) Yuda anapokea kikosi cha maaskari tayari kwa kumsaliti Bwana wake, Mwalimu na Muumba wake. Hapa naomba niseme kidogo, kwa utamaduni wa ...