Tetesi za Soka Ulaya Ijumaa 21.02.2020: Skriniar, Tah, Alonso, Klopp, Hodgson, Lallana
Haki miliki ya picha AFP Image Mshirikishe mwenzako Haki miliki ya picha AFP Image caption Wachezaji wa Atletico wanamtaka Jurgen Klopp kutizama mapungufu ya timu yake badala ya kuwakosoa. Wachezaji wa Atletico Madrid walishikwa na hasira na kushangazwa baada ya kukosolewa na kocha wa Liverpool Jurgen Klopp. Atletico iliwafunga Liverpool 1-0 Jumanne katika raundi ya kwanza ya hatua ya mtoano ya Kombe la Mabingwa Ulaya, wachezaji wa Atletico wanamtaka Klopp kutizama mapungufu ya timu yake badala ya kuwakosoa. (ESPN) Manchester City na Barcelona wanaminyana kumsajili beki wa Inter Milan na Slovakia Milan Skriniar, 25, na klabu itakayofanikiwa kumnyakua itabidi itoe dau la zaidi ya pauni milioni 75. (Calciomercato) Arsenal wanapanga kumsajili beki wa Bayer Leverkusen na Ujerumani Jonathan Tah ambaye kwa mujibu wa mkataba wake anathamani ya pauni milioni 34. (Bild - in German) Haki miliki ya picha TF-IMAGES Image caption Jonathan Tah Beki wa pembeni wa Chelsea Marcos Alonso, 29, bado yu...