Paul Kagame afanya mabadiliko makubwa baraza la mawaziri, amuondoa kazini waziri wa ulinzi Rwanda
Paul Kagame afanya mabadiliko makubwa baraza la mawaziri, amuondoa kazini waziri wa ulinzi Rwanda Haki miliki ya picha AFP/GETTY IMAGES Rais wa Rwanda Paul Kagame amefanya mabadiliko makubwa katika baraza lake la mawaziri na kumteua Dkt Richard Sezibera kuwa waziri mpya wa mashauri ya nchi za nje. Jenerali James Kabarebe aliyekuwa mtu wa karibu sana na Rais Kagame amepoteza wadhifa wake kama waziri wa ulinzi na badala yake akateuliwa mshauri wa rais katika masuala ya usalama. Kagame: Raia wa Rwanda walitaka wenyewe Diane Rwigara na mamake waachiliwa huru Rwanda Je Victoire Ingabire ni nani? Tanzania inashikilia nafasi ya ngapi kwa utajiri Afrika? Katika mabadiliko makubwa na ya kushtukiza aliyofanya Rais Kagame wizara 8 kati ya 23 zimepata mawaziri wapya zikiwemo wizara nyeti tatu, wizara ya ulinzi ambayo sasa inaongozwa na Meja jenerali Albert Murasira aliyechukua nafasi ya Jenerali James Kabarebe. Mwandishi wa BBC Yves Bucyana anasema si wengi walitarajia mab...