Posts

Showing posts from April, 2018

Fahamu nchi zinazotumia bangi kwa kiasi kikubwa DUNIANI

Image
Fahamu nchi zinazotumia bangi kwa kiasi kikubwa Haki miliki ya picha GETTY IMAGES Image caption Nchi nyingi barani Afrika ni kinyume cha sheria kulima, kuuza au kutumia bangi Lesotho Matumizi ya bangi nchini Lesotho yanaruhusiwa tu kwa matumizi ya dawa , kwa kiasi kikubwa bangi hulimwa nchini humo.Miaka ya 2000 ilikadiriwa kuwa asilimia 70 ya bangi nchini Afrika Kusini inatoka nchini Lesotho. Wakulima nchini Lesotho wanalima bangi kwa ajili ya matumizi yao nyumbani na kusafirisha nje ya mipaka, kutokana na hali ya umasikini waliyonayo, wakulima wadogo nchini humo wanalima bangi miongoni mwa mazao yao mengine kama vile mahindi kwa ajili ya kusafirisha nchini Afrika Kusini. Zimbabwe kuhalalisha upanzi na matumizi ya bangi Afrika Kusini Afrika Kusini ni nchi ambayo ilitarajiwa kuwa ya kwanza kuhalalisha bangi.Mwezi Aprili mwaka jana, ilihalalisha bangi kwa matumizi binafsi nyumbani, lakini haikuruhusiwa kuzalishwa au kuuzwa. Tangu mwezi machi mwaka 2017, ba...

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO MEI MOSI yaliyomo lissu Nimesahau kutembea ajiandaa kufanyiwa upasuaji wa 20

Image

RAISI WA WANYONGE

https://youtu.be/Q1HXluulllg

Magufuli azindua ukuta Mererani, amtambua mvumbuzi wa Tanzanite Jumanne Ngoma

Image
lymoson@ Haki miliki ya picha AFP Image caption Rais Magufuli aliagiza kujengwa ukuta kuzunguka mgodi wa Tanzanite mwaka jana Rais John Magufuli wa Tanzania,amezindua ukuta wa machimbo ya madini ya Tanzanite, yaliyopo eneo la Mererani, kaskazini mwa nchini Tanzania. Ukuta huo ulijengwa ili kuzuia wachimbaji madini kukwepa kulipia ushuru na kuiba madini. Rais Magufuli amesema hatosita kuzungushia ukuta sehemu yoyote yenye rasimali ambayo inaleta utata, hata ikiwa mlima Kilimanjaro yupo radhi kuulinda kwa kujenga ukuta. Hata hivyo, Magufuli alitambua uwepo wa mvumbuzi wa kwanza wa madini ya Tanzanite ambaye hakuwahi kutambuliwa na taifa. Bwana Jumanne Mhero Ngoma alivumbua aina hiyo ya dini la Tanzanite mwaka 1967. Image caption Bwana Jumanne Mhero Ngoma alivumbua dini la Tanzanite mwaka 1967. Jumannne Ngoma ametambuliwa na Rais Magufuli na amemzawadia shujaa huyo milioni 100 kwa ajili ya kumsaidia kujikimu na matibabu baada ya mzee huyo kupooza sehemu ya mwili. Aliw...

Mwanamume atolewa mswaki tumboni Mombasa, Kenya

Image
Haki miliki ya picha HISANI Madaktari katika Hospitali Kuu ya Mkoa ya Pwani (CPGH) mjini Mombasa, Kenya wamefanikiwa kuutoa mswaki ambao ulikuwa umekwama tumboni mwa mwanamume mmoja kwa siku sita. David Charo alikuwa akipiga mswaki alipoumeza kimakosa Jumapili wiki iliyopita apokuwa anajiandaa kwenda kazini Bamba, Kilifi. Kufikia jana, alikuwa ameanza kupata matatizo ya kupumua. Awali, madaktari walikuwa wamedokeza kwamba angehitaji kufanyiwa upasuaji kuutoa. Lakini Ijumaa asubuhi, madaktari wakiondozwa na Ramadhan Omar wamefanikiwa kuutoa mswaki huo bila kumfanyia upasuaji wa kawaida. Badala yake, wamemfanyia upasuaji wa kutumia matundu madogo. Jumapili, Charo alipokuwa alipoumeza mswaki huo kimakosa, awali ulikwama ndani ya koo kabla ya kutumbukia ndani tumboni. Haki miliki ya picha AFP Juhudi za nduguye mdogo Julius Charo za kuutoa hazikufanikiwa na ikalazimu wamkimbize hospitali iliyokuwa karibu. "Tulipompeleka kwenye hospitali hiyo, madaktari walitusha...