MAMBO MATANO KUHUSU DOMINIKA YA MATAWI
MAMBO 5 KUHUSU DOMINIKA YA MITI YA MITENDE [MATAWI] YANAYOTUKUMBUSHA KUWA KRISTO NI MFALME. [Share] Dominika ya Miti ya Mitende ni sikukuu ya Kikristo inayohamishika kulingana na tarehe ya Pasaka, na huadhimishwa Jumapili iliyotangulia Pasaka. Sikukuu hii huadhimisha kuingia kwa Yesu kwa shangwe mjini Yerusalemu, tukio lililotajwa katika Injili zote nne. Dominika hii pia huashiria mwanzo wa Juma Takatifu. Inaitwa Dominika ya Miti ya Mitende kwa sababu matawi ya mitende hubarikiwa na kubebwa kwa maandamano kuenzi kuingia kwa Bwana Yesu Yerusalemu. Ni Jumapili pekee ambapo Injili mbili tofauti husomwa. Injili ya mateso (Passion) ndiyo ndefu zaidi ya mwaka. Misa hii huwa na hisia mbili zinazotofautiana sana—mwanzo wa shangwe, lakini baadaye huzuni kuu. Yesu aliingia Yerusalemu kwa furaha kubwa, watu wakimpigia kelele za "Hosana", lakini muda mfupi baadaye hali ikawa ya huzuni—kwanza na yule Mtumishi anayeteseka aliyetoa mgongo wake kwa wapigao (Isaya 50:6), kisha Yesu mwenyewe ...